• HABARI MPYA

    Friday, June 02, 2017

    KHAMIS MCHA ''VIALLI' ATUPIWA VIRAGO AZAM FC

    Na Shekha Jamal, DAR ES SALAAM
    UONGOZI wa Azam FC, umeweka wazi kimtema mchezaji wake Khamis Mcha 'Vialli', baada ya kumaliza mkataba wake na timu hiyo.
    Akizungumza na Waandishi wa habari, Ofisa habari wa Azam, Jaffer Iddi alisema benchi la ufundi limetoa repoti ya kutoendelea na mchezaji huyo.
    Alisema mbali na mchezaji huyo pia Ame Ally amemaliza mkataba na hawataendelea tea.
    Ame ambaye alikwenda kwa mkopo Simba na msimu huu kucheze Kagera Sugar ambao wamemaliza Ligi Kuu Tanzania Bara.
    Khamis Mcha 'Vialli' ametemwa Azam FC baada ya kumaliza mkataba wake 

    "Kwa sasa wachezaji hao sio wa Azam na kuitakia baraka huko waendako, pia suala la Aishi Manula na Shomari Kapombe wako katika mazungumzo," alisema.
    Jaffer alisema wachezaji hao wakitoka katika kikosi cha Taifa Stars watakaa meza moja na kusaini mikataba mipya.
    Alisema katika usajili mpya alisema wanakuwa makini katika usajili wa wachezaji wa ndani kulingana na mahitaji ya benchi la ufundi.
    " Mazoezi tunaanza rasmi Julai 9 mwaka huu na timu tutakaa katika hostel zetu zilizopo Chamazi, hatutakwenda nje ya nchi," alisema
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KHAMIS MCHA ''VIALLI' ATUPIWA VIRAGO AZAM FC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top