• HABARI MPYA

    Thursday, June 29, 2017

    STARS YATINGA ROBO FAINALI COSAFA, KUCHEZA NA BAFANA JUMAPILI

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    TANZANIA imekwenda Robo Fainali ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Kusini mwa Afrika (COSAFA) Castle baada ya sare ya 1-1 na Mauritius jioni ya leo Uwanja wa Moruleng mjini Rusternburg, Afrika Kusini.
    Pongezi kwake winga Simon Happygod Msuva aliyetokea benchi kipindi cha pili na kwenda kuifungia Taifa Stars bao la kusawazisha dakika ya 68, dakika moja tu baada ya Kevin Perticots aliyetokea benchi pia kuifungia bao la kuongoza Mauritius.
    Kwa matokeo hayo, Tanzania itamenyana na wenyeji, Afrika Kusini 'Bafana Bafana' Jumapili Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace katika Robo Fainali.
    Timu nyingine zilizofuzu katika hatua hiyo ni Botswana, Zambia, Namibia, Lesotho na Swaziland zilizoanzia hatua hiyo na zitamsubiri mshindi wa Kundi B kesho kukamilisha ‘Nane Bora’ za COSAFA 2017.
    MISIMAMO YA MAKUNDI
    Kundi A                    P          W        D         L          GF       GA       Pts
    Tanzania
                       3          1          2         0          3          1          5
    Angola                      3          1          2         0          1          0          5
    Mauritius                  3          0          2         2          1          1          2
    Malawi                      3          0          2         1          0          2          2
    Kundi B                     P        W        D         L          GF       GA       Pts
    Zimbabwe                2         1         1          0          4          0          4
    Madagascar             2         1         1          0          2          0          4
    Msumbiji                   2         1          0         1          2          5          3
    Shelisheli                  2         0          0         2          1          4          0
    Na hiyo ni baada ya kumaliza na pointi tano sawa na Angola, lakini Taifa Stars inabebwa na wastani wake mzuri wa mabao, huku Mauritius na Malawi zote zikimaliza na pointi mbili kila moja.
    Kundi B hadi sasa, Zimbabwe inaongoza kwa wastani wa mabao tu, ikiwa na pointi nne sawa na Madagascar, wakati Msumbiji ina pointi tatu na Shelisheli haina kitu.   
    Mauritius leo ilimaliza pungufu baada ya mchezaji wake, Damien Balisson kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 78, lakini Tanzania ikashindwa kutumia mwanya huo kuongeza mabao.
    Kikosi cha Tanzania kilikuwa; Aishi Manula, Hassan Kessy, Gardiel Michael, Abdi Banda, Salim Mbonde, Erasto Nyoni, Himid Mao, Shiza Kichuya, Elias Maguri/Simon Msuva dk58 na Thomas Ulimwengu.
    Malawi; K. Jean-Louis, M. Dorza, E. Vincent-Jean, D. Balisson, C. Bell, L. Rose, A. Langue/J.Jocelyn dk87, L. Rungassamy/K. Perticots dk46, J. Villeneuve, W. St Martin/K. Saramandif dk77 na F. Rasolofonirina.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: STARS YATINGA ROBO FAINALI COSAFA, KUCHEZA NA BAFANA JUMAPILI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top