• HABARI MPYA

    Friday, April 07, 2017

    MWAMBUSI: YANGA TUKO TAYARI KUWAZIMA WAARABU KESHO

    Na Rehema Lucas, DAR ES SALAAM
    KOCHA Msaidizi wa Yanga, Juma Mwambusi amesema kwamba wachezaji wao wako tayari kwa mchezo wa kwanza wa mchujo wa kuwania kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho la Afrika dhidi ya Mouloudia Club Alger ya Algeria kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 
    Akizungumzia mchezo huo leo, Mwambusi alisema wamefanya mazoezi yao ya mwkisho asubuhi ya leo na sasa wanahamishia nguvu na fikra zao kwenye maandalizi ya kisaikolojia kwa saa zilizobakia.
    “Wachezaji wa Yanga wako na morali wa hali juu na kikubwa tunawaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu hii kwa sababu ni klabu pekee iliyobaki ikiiwakilisha nchi,”alisema.
    Juma Mwambusi amesema wako tayari kwa mchezo na Mouloudia Club Alger kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam

    Mchezo huo utachezeshwa na marefa kutoka Rwanda, Louis Hakizimana ambaye atakuwa mwamuzi wa kati akisaidiwa na Theogene Ndagijimana akiwa mshika kibendera wa mstari wa kulia na Jean Bosco Niyitegeka ambaye atakuwa mshika kibendera mstari wa kushoto. 
    Mwamuzi wa akiba ambaye pia atakuwa anatokea Rwanda ni Ruzindana Nsoro wakati Kamishna wa mchezo atakuwa Ata Elmanan Hassan Osama kutoka Sudan. Waamuzi hao pamoja na Kamishna wa mchezo wamefikia Hoteli ya Urban Rose iliyoko Mtaa wa Jamhuri, katikati ya jiji la Dar es Salaam, Tanzania.  
    Wapinzani wa Yanga, MC Alger waliingia jana usiku saa 3.30 kutoka Algeria kwa ndege maalumu ya kukodi na kufikia Hoteli ya Holiday Inn na leo jioni wanafanya mazoezi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.  
    Viingilio vya vimepangwa kuwa Sh 30,000 kwa VIP ‘A’; Sh 20,000 kwa VIP ‘B’ na ‘C’ wakati mzungunguko itakuwa ni Sh 3,000.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MWAMBUSI: YANGA TUKO TAYARI KUWAZIMA WAARABU KESHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top