• HABARI MPYA

    Saturday, April 22, 2017

    CHELSEA YAIFUMUA SPURS 4-2 NA KWENDA FAINALI KOMBE LA FA ENGLAND

    Eden Hazard akiteleza chini kushangilia baada ya kuifungia bao la tatu Chelsea dakika ya 75 katika ushindi wa 4-2 dhidi ya Tottenham Hotspur leo Uwanja wa Wembley katika Nusu Fainali ya Kombe la FA England. Willian amefunga mabao mawili moja dakika ya tano na lingine dakika ya 43 kwa penalti wakati bao lingine la Chelsea limefungwa na Nemanja Matic dakika ya 80 huku ya Spurs yakifungwa na Harry Kane dakika ya 18 na Dele Alli dakika ya 52. Chelsea sasa itakutana na mshindi kati ya Arsenal na 
    Manchester City zinazomenyana kesho Wembley PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: CHELSEA YAIFUMUA SPURS 4-2 NA KWENDA FAINALI KOMBE LA FA ENGLAND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top