• HABARI MPYA

    Friday, September 23, 2016

    SIMBA SC YAWAAMBIA MAJIMAJI KIFO LAZIMA TU KESHO WATAKE WASITAKE

    RATIBA YA LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA…
    Septemba 24, 2016
    JKT Ruvu Vs Mbeya City
    Simba Vs Maji Maji
    Ndanda Vs Azam FC
    Prisons Vs Mwadui
    Mtibwa Sugar Vs Mbao
    Septemba 25, 2016
    Ruvu Shooting Vs Toto Africans
    Stand United Vs Yanga SC
    African Lyon Vs Kagera Sugar

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    WAKATI Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inaendelea kesho, Simba SC imewaambia Maji Maji watakufa wapende wasipende.
    Simba SC watakuwa wenyeji wa Maji Maji kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mfululizo wa ligi hiyo na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Hajji Sunday Manara amesema; “Ushindi lazima kesho, Maji Maji watakufa watake wasitake”.
    Akizungumza na BIN ZUBEIRY SPORTS – ONLINE leo, Manara amewataka mashabiki na wapenzi wa klabu hiyo kujitokeza kwa wingi kesho kuisapoti timu yao.
    “Nichukue nafasi hii kuwaomba wana Simba wajitokeze kwa wingi kesho katika mchezo wetu na Maji Maji, kwani tuna matumaini makubwa ya kuendeleza wimbi la ushindi,”alisema Manara.
    Kiungo Mwinyi Kazimoto Mwitula anatarajiwa kurejea kwenye mchezo wa kesho baada ya kukosekana katika mchezo uliopita wakishinda 1-0 dhidi ya Azam FC kutokana na kuwa majeruhi.
    Mshambuliaji Ibrahim Hajib aliyetiliwa shaka ya maumivu yuko vizuri na anaweza kucheza pia kesho.
    Kwa ujumla Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea wikiendi hii kwa timu zote kuingia viwanjani kusaka pointi.  
    JKT Ruvu Stars wanatarajiwa kuwa wenyeji wa Mbeya City Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani, Ndanda wanatarajiwa kuwa wenyeji wa Azam FC Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara, Prisons wataikaribisha Mwadui FC Uwanja wa Sokoine, Mbeya na Mtibwa Sugar watakuwa wenyeji wa Mbao FC Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro.
    Ligi Kuu itaendelea Jumapili, Ruvu Shooting wakiikaribisha Toto Africans Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani, Stand United wakimenyana na Yanga SC Uwanja wa Kambarage, Shinyanga na African Lyon wakiwa wenyeji wa Kagera Sugar Uwanja wa Taifa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC YAWAAMBIA MAJIMAJI KIFO LAZIMA TU KESHO WATAKE WASITAKE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top