• HABARI MPYA

    Friday, April 08, 2016

    YANGA WAIGOMEA AHLY KUONYESHA MECHI MISRI

    Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
    UONGOZI wa Yanga umegoma kuwauzia wapinzani wao, Al Ahly ya Misri haki za kurusha matangazo ya mechi baina yao kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Yanga watakuwa wenyeji wa Ahly kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa kwanza hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Afrika na Ahly walitaka wachukue matangazo kwa ajili ya kurusha Misri tu.
    Hata hivyo, leo uongozi wa Ahly umethibitisha rasmi kwamba umenyimwa haki hiyo na utaonyesha mechi hiyo kupitia mitandao tu.
    Yanga na Al Ahly wanakutana katika marudio ya mechi ya mwaka 2014
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA WAIGOMEA AHLY KUONYESHA MECHI MISRI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top