• HABARI MPYA

    Sunday, March 20, 2016

    AFRICAN SPORTS YALALA 1-0 MKWAKWANI

    MATOKEO NA RATIBA LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA
    Machi 20, 2016
    African Sports 0-1 Prisons
    Machi 19, 2016
    Coastal Union 0-2 Simba SC
    Majimaji 3-1 Mbeya City
    Stand United 1-1 Ndanda FC
    Machi 14, 2016
    African Sports 2-0 Mbeya City
    Machi 18, 2016
    Kagera Sugar 1-0 Mtibwa Sugar
    Kesho; Machi 21, 2016
    Mgambo JKT Vs Toto Africans
    Machi 24, 2016
    African Sports Vs Toto Africans
    African Sports imefungwa 1-0 na Prisons leo Uwanja wa Mkwakwani, Tanga

    AFRICAN Sports imezidi kujiweka katika mazingira ya kushuka daraja baada ya kufungwa 1-0 nyumbani na Prisons ya Mbeya jioni ya leo katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
    Bao pekee la Prisons leo limefungwa na beki James Mwasote sekunde ya 46 dakika ya kwanza aliyepiga kona iliyoingia moja kwa moja nyavuni, ingawa ilisindikizwa na Jumanne Elfadhil wakati tayari imekwishaingia langoni.
    Kwa ushindi huo, Prisons inafikisha pointi 39 baada ya kucheza mechi 24 ingawa inaendelea kukamata nafasi ya tano, nyuma ya Mtibwa Sugar yenye pointi 39 pia na wastani mzuri wa mabao.
    Kwa African Sports, inabaki na pointi zake 20 za mechi 24 na kuendelea kushika nafasi ya 15 katika ligi ya timu 16, mbele ya ndugu zao, Coastal Union wenye pointi 19 za mechi 24 pia.
    Sports iliyopanda Ligi Kuu msimu huu baada ya zaidi ya miaka 20, sasa inahitaji kufanya kazi ya ziaba ili kubaki kwenye ligi hiyo, sawa na ndugu zao, Coastal na JKT Mgambo – ambao kwa pamoja wanashika nafasi tatu za mwisho.
    Ligi Kuu inatarajiwa kuendelea kesho Uwanja wa Mkwakwani, kwa timu nyingine ya Tanga, JKT Mgambo kuikaribisha Toto Africans ya Mwanza.
    Mgambo inashika nafasi ya 14 kwa pointi zake 20 za mechi 23, wakati Toto ni ya 12 ikiwa na pointi 23 za mechi 22.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AFRICAN SPORTS YALALA 1-0 MKWAKWANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top