• HABARI MPYA

    Monday, January 15, 2018

    REFA AMPIGA TEKE MCHEZAJI UFARANSA NA KUMPA KADI NYEKUNDU

    REFA Mfaransa, Tony Chapron usiku wa jana amefanya kituko cha aina yake baada ya kumpiga teke beki wa Nantes, Diego Carlos kabla ya kumuonyesha kadi ya pili ya njano na kumtoa kwa nyekundu dakika ya 90 na ushei timu yake ikifungwa 1-0 na  Paris Saint-Germain katika mechi ya Ligue 1 Uwanja wa Beaujoire - Louis Fonteneau mjini Nantes.
    Carlos alikuwa tayari ana kadi ya njano wakati Paris Saint-Germain wanapeleka shambulizi la kujibu na mchezaji huyo Mbrazil mwenye umri wa miaka 24 akagongana na refa huyo wakati anakimbia kurudi kuihami timu yake isifungwe.
    Refa alikuwa anakimbia na mchezo na bahati mbaya akapamiana na Mbrazil huyo na kuanguka chini, lakini ajabu akainuka na kumrudishia kwa teke kabla ya kumuonyesha kadi mfululizo.
    Refa Tony Chapron akimuonyesha kadi nyekundu, beki wa Nantes, Diego Carlos jana

    Beki wa Nantes alionyesha uungwana kwa kumsaidia refa Chapron baada ya kuanguka, ingawa hiyo haikumsaidia kumuepusha na kadi na akawapa mpira wa adhabu PSG wapige. 
    PSG iliibuka na ushindi wa 1-0 kwenye mchezo huo, bao pekee la winga Muargentina, Angel Di Maria dakika ya 12.
    Rais wa Nantes, Waldemar Kita ametaka refa Chapron afungiwe miezi sita.
    "Nimepokea SMS 20 duniani kote zikiniambia huyu refa ni wa ovyo,"alisema Kita akizungumza na L'Equipe.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: REFA AMPIGA TEKE MCHEZAJI UFARANSA NA KUMPA KADI NYEKUNDU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top