• HABARI MPYA

    Tuesday, January 23, 2018

    MGOYI KUSIMAMIA MECHI YA AFC LEOPARDS NA TIMU YA MADAGASCAR KOMBE LA SHIRIKISHO

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limemteua Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Ahmed Iddi 'Msafiri' Mgoyi kuwa Kamishna wa mchezo wa Kombe la Shirikisho kwa klabu kati ya AFC Leopards ya Kenya na Fosa Juniors ya Madagascar.
    Mchezo huo namba 13 utachezwa nchini Kenya kati ya Februari 9,10 na 11 mwaka huu.
    Kwenye mchezo huo waamuzi wote wanatoka nchini Somalia ambapo mwamuzi wa kati ni Abdulkadir Artan Omar,mwamuzi msaidizi namba moja Ali Mohamed Mahad,mwamuzi msaidizi namba mbili Ahmed Abdullah Farah wakati mwamuzi wa akiba ni Hassan Mohamed Hagi.
    Ahmed Mgoyi (kushoto) atakuwa Kamishna wa mchezo wa Kombe la Shirikisho kati ya AFC Leopards ya Kenya na Fosa Juniors ya Madagascar

    Mgoyi ni miongoni mwa Wajumbe wa Kamati ya utendaji wa TFF walioteuliwa hivi karibuni kuwa makamishna wa mechi zinazoandaliwa na CAF kwa mwaka 2018 mpaka mwaka 2020 wengine ni Makamu wa Rais wa TFF Michael Wambura,Amina Karuma na Sarah Tchao.
    Aidha Rais wa TFF Ndugu Wallace Karia naye mbali ya kuteuliwa kwenye kamati ya mashindano ya fainali za Africa kwa wachezaji wanaocheza ndani CHAN tayari amechaguliwa mara mbili kusimamia mechi za CHAN zinazoendelea nchini Morocco.
    Alisimamia mechi ya ufunguzi iliyowakutanisha Wenyeji Morocco na Mauritania Januari 13, 2018 na mchezo wa pili uliochezwa jana Januari 22, 2018 kati ya Namibia na Zambia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MGOYI KUSIMAMIA MECHI YA AFC LEOPARDS NA TIMU YA MADAGASCAR KOMBE LA SHIRIKISHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top