• HABARI MPYA

    Tuesday, January 23, 2018

    UNAOWAONA NI MABOSI WA ARSENAL WANASHANGAA GARI LA AUBAMEYANG UJERUMANI

    Mtendaji Mkuu wa Arsenal, Ivan Gazidis na Mkuu wa Usajili, Sven Mislintat wakilishangaa gari la Aubameyang aina ya Porsche Panamera PICHA ZAIDI GONGA HAPA  


    Porsche Panamera Turbo Techart 

    GHARAMA: Pauni 132,000
    UFUFUJI: 0-60mph in 3.9secs
    SPIDI: 182mph  
    MSAFARA wa Arsenal uliotumwa kwenda kushughulikia usajili Pierre-Emerick Aubameyang kutoka Borussia Dortmund umejionea mfumo wa maisha ya kifahari ya mchezaji huyo.
    Mtendaji Mkuu wa Arsenal, Ivan Gazidis na Mkuu wa Usajili, Sven Mislintat walipigwa picha mjini Dortmund wakiondoka kwenye gari kuingia kwenye mkutano na viongozi wenzake wa timu ya Ujerumani kuzungumzia uhamisho wa mchezaji huyo kumpelekea Ligi Kuu ya England.
    Na picha zimetokea zikiwaonyesha Gazidis na Mislintat wakizungumza na kulishangaa gari la kifahari aina ya Porsche Panamera Turbo Techart ambalo linamilikiwa na Aubameyang, mtu wanayetumaini kurejea naye Arsenal.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: UNAOWAONA NI MABOSI WA ARSENAL WANASHANGAA GARI LA AUBAMEYANG UJERUMANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top