TIMU ya Simba SC imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la Muungano baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya wenyeji, Mlandege FC usiku huu Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
Mabao ya Simba SC yamefungwa na mshambuliaji mzawa, Suleiman Abdallah Mwalimu ‘Gomez’ dakika ya 61, winga Muivory Coast, Alain Anicet Oura dakika ya 76 na kiungo wa Kimataifa wa Afrika Kusini, Neo Gift Maema dakika ya 89.
Simba SC itakutana na mtani wake, Simba SC katika Fainali ya Kombe la Muungano 2026 Jumatano, Aprili 29 kuanzia Saa 2:15 usiku hapo hapo New Amaan Complex.
Ikumbukwe jana mabingwa hao, watetezi, Yanga SC walifanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la Muungano baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Azam FC hapo hapo Amaan Complex.
Hii ni maana yake miamba hiyo ya soka nchini italutana mara mbili ndani ya wiki moja, kwani Mei 3 watamenyana katika mechi ya marudiano ya Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara kuanzia Saa 12:00 jioni Uwanja wa Meje Jenerali Isamuhyo, Mbweni, Dar es Salaam.



.png)
0 comments:
Post a Comment