TIMU ya Mlandege FC imetinga Nusu Fainali ya Kombe la Muungano baada ya us Hindi wa mabao 2-1 dhidi ya Singida Black Stars jioni ya leo Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
Mabao ya Mlandege yamefungwa na Omar Juma’Samatta’ dakika ya 28 na Mussan Hassan ‘Mbappe’ dakika ya 45’+1, baada ya Mishamo Daudi kuanza kuifungia Singida Black Stars dakika ya tisa.
Mlandege sasa itakutana na mshindi kati ya Simba SC na Mafunzo FC zinazocheza baadaye leo kuanzia Saa 2:15 usiku hapo hapo Uwanja Amaan.



.png)
0 comments:
Post a Comment