KOCHA wa Manchester United, Mreno Jose Mourinho amesema atatumia beki mmoja na washambuliaji tosa katika mchezo wa Ligi Kuu ya Englamd dhidi ya Liverpool kesho Uwanja wa Anfield.
Mourinho alishambuliwa kwa 'kupaki basi' katika mchezo dhidi ya kikosi cha Jurgen Klopp wakitoa sare ya bila kufungana Merseyside mwaka mmoja uliopita.
Na baada ya kuulizwa maswali katika mkutano na Waandishi wa Habari leo kuelekea mchezo wa kesho, Mourinho alisema; "Tutacheza na mtu mmoja nyuma kisha tunakuja na mfumo mpya na tutacheza na washambuliaji tisa, usihofu juu ya hili," alisema Mourinho.
Jose Mourinho amesema atatumia beki mmoja na washambuliaji tisa katika dhidi ya Liverpool
0 comments:
Post a Comment