• HABARI MPYA

    Wednesday, October 25, 2017

    HIVI NDIVYO SIMBA WALIVYOMDHIBITI AJIB MECHI YA NGAO, JUMAMOSI ITAKUWAJE?

    Beki wa Simba, Salim Mbonde akimzuia kwa mkono mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajib asikamilishe mpango wake wa kumpiga chenga ya kumzunguka katika mchezo wa Ngao ya Jamii Agosti 23, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Ibrahim Ajib akijitahidi kujinasua kwenye mkono wa Salim Mbonde auwahi mpira katika mchezo ambao ilishinda kwa penalti baada ya sare ya 0-0
    Salim Mbonde hapa akiondosha mpira kwenye hatari dhidi ya Ibrahim Ajib. Wakati timu hizo zitamenyana tena Jumamosi Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, Mbonde hatakuwepo kutokana na kuwa majeruhi
    Agosti 23 Ibrahim Ajib aliwekewa ulinzi mkali na wachezaji wa Simba, hapa akikwatuliwa na Muzamil Yassin
    Ibrahim Ajib hapa akiwatoka Erasto Nyoni na Haruna Niyonzima
    Ibrahim Hajib hapa amewaunga msafara Method Mwanjali na Ally Shomari
    Hapa Ibrahim yuko chini ya uangalizi wa Method Mwanjali. Jumamosi itakuwaje?
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HIVI NDIVYO SIMBA WALIVYOMDHIBITI AJIB MECHI YA NGAO, JUMAMOSI ITAKUWAJE? Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top