• HABARI MPYA

    Friday, September 20, 2019

    WILKER DA SILVA AFUNGA SIMBA SC IKIICHAPA AZAM B 3-0 MECHI YA KIRAFIKI MAZOEZINI LEO DAR

    Mshambuliaji Mbrazil wa Simba SC, Wilker Henrique da Silva akiwapangua wachezaji wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Azam FC katika mchezo wa kirafiki Uwanja wa Gymkhana mjini Dar es Salaam leo asubuhi. Simba imeshinda 3-0 mabao yake yakifungwa na kiungo Msudan, Sharaf Eldin Shiboub, Wilker da Silva na beki mzawa, Kennedy Wilson     
    Beki wa kati wa Simba SC, Kennedy Wilson (kulia) akitafuta mbinu za kuwapita wachezaji wa Azam   
    Beki wa Simba SC, Gerson Fraga Vieira akitafuta namna ya kumpita mchezaji wa Azam FC  
    Beki Muiviory Coast, Serge Pascal Wawa akimdhibiti mchezaji wa Azam FC  
    Beki wa kulia, Shomary Kapombe akitafuta namna ya kuwapita wachezaji wa Azam FC
    Kiungo Ibrahim Ajibu akimiliki mpira katikati ya wachezaji wenzake
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WILKER DA SILVA AFUNGA SIMBA SC IKIICHAPA AZAM B 3-0 MECHI YA KIRAFIKI MAZOEZINI LEO DAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top