• HABARI MPYA

    Sunday, September 29, 2019

    TANZANIA BARA YAIPIGA UGANDA 4-2, KUIVAA SUDAN NUSU FAINALI CECAFA U20

    Na Mwandishi Wetu, GULU
    TIMU ya Tanzania Bara imefanikiwa kuingia Nusu Fanali ya michuano ya Kombe la Matafa ya Afrika Masharki na Kati (CECAFA Challenge U20) baada ya ushind wa 4-2 dhidi ya wenyeji, Uganda jioni Uwanja wa Kumbukumbu wa Gulu.
    Mabao ya Tanzania Bara leo yamefungwa na washambuliaji wake hodari, Andrew Albert Simchimba dakika za 25 na 62 na Kelvin Pius John ‘Mbappe’ dakika za 89 na 90 na ushe, wakati ya Uganda yamefungwa na Aziz Kayondo dakika ya 46 na 76. 
    Robo Fainali nyingine Sudan imefunga 1-0 Sudan Kusini Uwanja wa Gulu pia, Kenya imefunga Burundi 2-1 na Eritrea imeiadhibu 5-0 Zanzibar Uwanja wa Njeru.

    Sasa Tanzania Bara itamenyana na Sudan katika Nusu Fainali Jumatano.
    Fainali ya michuano ya CECAFA Challenge U20 mwaka 2019 itapigwa Oktoba 5.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TANZANIA BARA YAIPIGA UGANDA 4-2, KUIVAA SUDAN NUSU FAINALI CECAFA U20 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top