• HABARI MPYA

    Monday, March 11, 2019

    BENZEMA APIGA MBILI, REAL MADRID YAAMKA NA KUICHAPA VALLADOLID 4-1

    Mshambuliaji Karim Benzema akishangilia baada ya kuifungia Real Madrid mabao mawili dakika za 51 kwa penalti na 59 akimalizia pasi ya Toni Kroos katika ushindi wa 4-1 dhidi ya wenyeji, Real Valladolid katika mchezo wa La Liga usiku wa jana Uwanja wa Manispaa wa Jose Zorrilla mjini Valladolid. Mabao mengine ya Real Madrid yalifungwa na Raphael Varane dakika ya 34 na Luka Modric dakika ya 85, wakati la Real Valladolid lilifungwa na Anuar Tuhami dakika ya 29. Kwa ushindi huo, Real Madrid inafikisha pointi 51 baada ya kucheza mechi 27, ingawa inabaki nafasi ya tatu sasa ikizidiwa pointi tano na Atlético Madrid wanaoshika nafasi ya pili nyuma ya Barcelona wanaoongoza kwa pointi zao 63 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BENZEMA APIGA MBILI, REAL MADRID YAAMKA NA KUICHAPA VALLADOLID 4-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top