• HABARI MPYA

    Tuesday, March 26, 2019

    RONALDO AUMIA, URENO SARE TENA KUFUZU EURO 2020

    Mshambuliaji wa Ureno, Cristiano Ronaldo akiugulia maumivu jana wakati wa mchezo wa Kundi B kufuzu Euro 2020 dhidi ya Serbia usiku wa jana Uwanja wa Luz mjini Lisbon timu hizo zikitoka sare ya 1-1 kufutia kuumia nyama za paja kabla ya kutolewa dakika ya 31 tu nafasi yake ikichukuliwa na Pizzi. Kwa sare ya pili mfululizo jana, Ureno inashika nafasi ya tatu kwa pointi zake mbili nyuma ya Luxembourg pointi tatu na Ukraine pointi nne. Na hiyo baada ya jana Ukraine kuwachapa wenyeji, Luxembourg 2-1 mjini Luxembourg katika mchezo mwingine wa kundi hilo 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO AUMIA, URENO SARE TENA KUFUZU EURO 2020 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top