• HABARI MPYA

    Wednesday, March 27, 2019

    QUAGLIARELLA APIGA MBILI ITALIA YASHINDA 6-0 KUFUZU EURO 2020

    Mkongwe Fabio Quagliarella akishangilia baada ya kuifungia mabao mawili Italia dakika za 35 na 45 na ushei yote kwa penalti katika ushindi wa 6-0 dhidi ya Liechtenstein kwenye mchezo wa Kundi J kufuzu Euro 2020 usiku wa jana Uwanja wa Ennio Tardini mjini Parma. Mabao mengine ya Italia yalifungwa na Stefano Sensi dakika ya 17, Marco Verratti dakika ya 32, Moise Kean dakika ya 69 na Leonardo Pavoletti dakika ya 76 na kwa ushindi huo The Azzurri inafikisha pointi sita kufuatia kushinda mechi zake zote mbili za mwanzo ikifuatiwa na Ugiriki yenye pointi nne. Mechi nyingine za kundi hilo jana Bosnia-Herzegovina ililazimishwa sare ya 2-2 Ugiriki mjini Zenica na Finland ikawachapa wenyeji, Armenia 2-0 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: QUAGLIARELLA APIGA MBILI ITALIA YASHINDA 6-0 KUFUZU EURO 2020 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top