• HABARI MPYA

    Saturday, March 23, 2019

    MBAPPE, GRIEZMANN WAFUNGA UFARANSA YASHINDA 4-1 UGENINI

    Mshambuliaji Kylian Mbappe akiifungia Ufaransa bao la nne dakika ya 87 usiku wa jana Uwanja wa Zimbru mjini Chisinau ikiwalaza wenyeji, Moldova 4-1 katika mchezo wa ufunguzi Kundi H kufuzu Euro 2020. Mabao mengine ya Ufarana yalifungwa na Antoine Griezmann dakika ya 24, Raphael Varane dakika ya 27 na Olivier Giroud dakika ya 36, wakati la Moldova lilifungwa na Vladimir Ambros dakika ya 89 na mchezo mwingine wa Kundi H, Iceland pia imeshinda ugenini 2-0 dhidi ya Andorra Uwanja wa Taifa mjini Andorra la Vella, mabao ya kiungo Birkir Bjarnason dakika ya 22 na mshambuliaji Vioar Orn Kjartansson dakika ya 80 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MBAPPE, GRIEZMANN WAFUNGA UFARANSA YASHINDA 4-1 UGENINI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top