• HABARI MPYA

    Thursday, January 18, 2018

    CHELSEA WASONGA MBELE KWA MATUTA KOMBE LA FA

    Kipa wa pili wa Chelsea, Willy Caballero akiokoa penalti ya kwanza ya Norwich iliyopigwa na Nelson Oliveira na kuiwezesha The Blues kushinda kwa penalti 5-3 baada ya sare ya 1-1 ndani ya dakika 120 Uwanja wa Stamford Bridge, London. Michy Batshuayi alianza kuifungia Chelsea dakika ya 55, kabla ya Jamal Lewis kuisawazishia Norwich dakika ya 90 na ushei.
    Waliofunga penalti za Chelsea ni Willian, David Luiz, Azpilicueta, N'Golo Kante na Eden Hazard wakati za Norwich zilifungwa na J. Maddison, M. Vrančić na Josh Murphy.
    Chelsea ilimaliza pungufu ya wachezaji wawili, baada ya Pedro (dakika ya 117 na Batshuayi (dakika ya 120) kutolewa kwa kadi nyekundu baada ya wote kuonyeshwa kadi za pili za njano na sasa itakutana na Newcastle katika raundi ya nne ya kombe la FA Jumapili ya Januari 27, mwaka hu PICHA ZAIDI GONGA HAPA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: CHELSEA WASONGA MBELE KWA MATUTA KOMBE LA FA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top