• HABARI MPYA

    Saturday, May 06, 2017

    YANGA ISINGESHINDA LEO, BOSSOU ANGEWAAMBIA NINI KWA KUKOSA BAO HILI LA WAZI

    Beki Mtogo wa Yanga, Vincent Bossou akijaribu bila mafanikio kumfunga kipa wa Prisons, Aaron Kalambo katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Wakati huo ilikuwa kabla ya Yanga kupata bao hata moja katika ushindi wake wa 2-0, wafungaji Amissi Tambwe na Obrey Chirwa
    Vincent Bossou akasogea pembeni ya lango baada ya kubanwa na kipa Aaron Kalambo, lakini akapiga nje 
    Alipata nafasi nzuri sana baada ya mabeki wa Prisons kumuacha wakidhani ameotea 
    Wazi kama Tambwe na Chirwa wasingefunga baadaye, Bossou angekuwa midomoni mwa mashabiki wa Yanga 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA ISINGESHINDA LEO, BOSSOU ANGEWAAMBIA NINI KWA KUKOSA BAO HILI LA WAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top