• HABARI MPYA

    Monday, May 29, 2017

    HAZARD MCHEZAJI BORA WA MSIMU CHELSEA, ASHINDA PIA BAO BORA

    Kiungo wa Chelsea, Eden Hazard akiwa ameshika tuzo ya Bao Bora la Msimu usiku wa jana PICHA ZAIDI GONGA HAPA  


    TUZO ZA CHELSEA 2017 

    Bao Bora la Msimu: Eden Hazard
    Mchezaji Bora wa Wachezaji: N'Golo Kante 
    Mchezaji Bora wa Kike: Karen Carney
    Mchezaji Bora wa Akademi: Mason Mount
    Mchezaji Bora wa Mwaka: Eden Hazard
    Tuzo Maalum: John Terry 
    KIUNGO wa Chelsea, Eden Hazard ameshinda tena Tuzo ya Mchezaji Bora wa Msimu wa katika klabu hiyo katika sherehe zilizofanyika usiku wa jana mjini London.
    Mbelgiji, ambaye pia ameshinda tuzo ya Bao Bora la Msimu katika sherehe zilizofanyika Battersea Evolution, huku N'Golo Kante akishinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Wachezaji. 
    Kocha Antonio Conte alikabidhi tuzo hiyo kubwa, ambayo hutokana na kura za mashabiki baada ya kutolewa kwa orodha ya mwisho akiingia na Cesar Azpilicueta, David Luiz na Kante. 
    Usiku huo ukakamilishwa kwa sherehe ya kumuaga Nahodha John Terry anayestaafu, ambaye alipewa tuzo maalum kuutambua mchango wake.
    Chelsea imemaliza msimu vizuri baada ya kubeba ubingwa wa Ligi Kuu ya England na kushika nafasi ya pili kwenye Kombe la FA.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HAZARD MCHEZAJI BORA WA MSIMU CHELSEA, ASHINDA PIA BAO BORA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top