Mshambuliaji wa Yanga Veterani, Bakari Malima 'Jembe Ulaya' akimtoka beki wa Bin Slum katika mchezo wa marudiano wa Kombe la Azam Fresco usiku wa leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Yanga ilishinda 3-1 na Malima aliyecheza mbele badala ya nafasi yake maarufu, beki alifunga mabao mawili, lingine likifungwa na Nsajigwa Shadrack, wakati bao la Bin Slum lilifungwa na Abuu Ramadhani 'Amokachi'. Yanga sasa inakwenda Nusu Fainali, huku Bin Slum ikiaga mashindano
Beki wa Yanga, Nsajigwa Shadrack akimuacha chini mchezaji wa Bin Slum |
Kiungo wa Yanga, Ally Yussuf 'Tigana' akiwatoka wachezaji wa Bin Slum |
Deo Lucas akimtoka beki wa Bin Slum |
Mshambuliaji wa Bin Slum, Abuu Ramadhani 'Amokachi' akifumua shuti katikati ya wachezaji wa Yanga |
Beki wa Yanga, Saleh Hilal akimtoka mchezaji wa Bin Slum |
Shadrack Nsajigwa akienda chini wakati akipambana na Nsa Job |
Kocha wa Bin Slum, Mohammed Bin Slum akiwa haamini macho yake |
Kikosi cha Bin Slum kilichopigwa 3-1 na jana |
Kikosi cha Yanga jana |
Kocha mwingine wa Bin Slum, Iddi Moshi alitolewa kwa kadi nyekundu kwa kuwatolea lugha chafu marefa jana |
0 comments:
Post a Comment