• HABARI MPYA

    Monday, April 18, 2016

    AZAM NA WAMOROCCO, YANGA NA WAMALI MICHUANO YA AFRIKA

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    WAKATI mechi ya Al Ahly na Yanga itachezeshwa na marefa wa Mali, mchezo wa timu nyingine ya Tanzania katika michuano ya Afrika, Azam FC dhidi ya Esperance utachezewa na marefa wa Morocco.
    Marefa wa nchi jirani na Tunisia, Morocco ndiyo watachezesha mechi ya marudiano hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho Afrika kati ya wenyeji, Esperance dhidi ya Azam FC ya Tanzania.
    Mechi hiyo itachezwa kesho Uwanja wa Olimpiki Novemba 7 mjini Rades na marefa watakuwa ni Redouane Jiyed atakayepuliza filimbi akisaidiwa na Mouhib Abdallah Filali na Essam Benbaoa wote wa Morocco.
    Marefa wa Mali watachezesha mechi kati ya Al Ahly na Yanga Jumatano mjini Cairo

    Azam FC inahitaji kuulinda ushindi wake wa kwenye mchezo wa kwanza wa 2-1 Dar es Salaam ili kusonga mbele katika mchujo wa kuwania kupangwa makundi ya ligi ndogo ya michuano hiyo.
    Mechi ya marudiano hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Afrika kati wenyeji Ahly na Yanga Uwanja wa Borg el Arab mjini Alexandria, Misri Jumatano utachezeshwa na marefa wa Mali.
    Marefa wa Morocco watachezesha mechi kati ya Esperance na Azam kesho

    Hao ni Mahamadou Keita atakayepuliza kipyenga akisaidiwa na Balla Diarra na Drissa Kamory Niare, wote wa Mali.
    Yanga inahitaji ushindi wa ugenini Jumatano ili kwenda hatua ya makundi ya michuano hiyo, baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza Dar es Salaam. 
    Iwapo Yanga itatolewa, itakwenda kumenyana na moja ya timu nane zilizofuzu kwenye Kombe la Shirikisho kuwania kupangwa kwenye makundi ya kucheza michuano hiyo ya pili kwa ukubwa ya CAF katika ngazi ya klabu. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM NA WAMOROCCO, YANGA NA WAMALI MICHUANO YA AFRIKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top