• HABARI MPYA

    Friday, September 07, 2012

    COASTAL UNION WAENDELEZA WIMBI LA USHINDI ZBAR

    Coastal Union

    Na Princess Asia
    BAO pekee la Jerry Santo kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar leo limeipa ushindi wa 1-0 Coastal Union katika mchezo wake wa kirafiki dhidi ya Zimamoto.
    Huo ulikuwa mchezo wa pili kwa Coastal katika ziara yao ya siku tano visiwani humo, kujiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, inayoanza wiki ijayo. Katika mchezo wa kwanza, mabingwa hao wa Bara 1988, waliichapa Super Falcon mabao 3-0, wafungaji Suleiman Kassim ‘Selembe’, Jerry Santo na Danny Lyanga na Jumapili Coastal watacheza mechi yao ya mwisho na Mafunzo.
    Wimbi hili la ushindi kwa Cosatal, linafuatia mwendo wa kusuasua kwenye michezo ya kirafiki ya awali, ilipofungwa mechi nne kati ya tano, kiasi cha kuibuka tetesi makocha Juma Mgunda na Msaidizi wake, Habib Kondo wanaweza kutupiwa virago.
    Ilifungwa na Azam FC 2-0 Uwanja wa Chamazi, ilifungwa 2-1 na Yanga Uwanja wa Taifa, ilifungwa 3-2 na Bandari mjini Mombassa, baadaye 2-0 Tanga, ilifungwa 2-1 na Polisi mjini Morogoro na yenyewe iliifunga JKT Oljoro 1-0 Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: COASTAL UNION WAENDELEZA WIMBI LA USHINDI ZBAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top