• HABARI MPYA

    Friday, September 28, 2012

    AZAM KURUDI KILELENI LIGI KUU LEO?

    Azam FC

    Na Prince Akbar
    LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, leo inaingia katika mzunguko wake wa nne kwa mechi za Super Weekend, ambazo zitaonyeshwa moja kwa moja na kituo cha Televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini.
    Mechi ya kwanza ambayo itachezwa leo itakuwa kati ya Azam FC na JKT Ruvu Stars, itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 1:00 usiku kwa viingilio vya Sh. 3,000 mzunguko, sh. 5,000 kwa VIP C na VIP B wakati VIP A kiingilio kitakuwa sh. 10,000.
    Kesho kutakuwa na mechi kati ya Simba na Tanzania Prisons itakayofanyika Uwanja wa Taifa, pia mjini Dar es Salaam kuanzia saa 11:00 jioni, wakati Yanga na African Lyon zitapambana keshokutwa kwenye Uwanja huo huo kuanzia saa 11:00 jioni.
    Uwanja wa Chamazi, maarufu kama Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam wenyewe utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar itakayochezwa Oktoba 1, mwaka huu kuanza saa 10:30 jioni.
    Mechi ya mwisho ya Super Weekend itachezwa Oktoba 3 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ikwakutanisha watani wa jadi, Yanga na Simba kuanzia saa 1:00 usiku.
    Wakati huo huo: Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Katibu Mkuu mstaafu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Erasto Zambi kilichotokea juzi mjini Dar es Salaam kutokana na maradhi.
    Zambi ambaye anatarajiwa kuzikwa Jumapili, kabla ya kuwa kiongozi TOC, kwa muda mrefu alikuwa mwalimu wa michezo katik Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambapo wanamichezo wengi hasa waliokuwa wanafunzi katika chuo hicho wamepita kwake.
    Msiba huo ambao uko nyumbani kwake Ubungo Kibangu, Dar es Salaam ni pigo kwa familia ya Zambi, TFF na wanamichezo kwa ujumla nchini kutokana na mchango na mawazo aliyotoa kwa shirikisho wakati akiwa kiongozi wa TOC.
    TFF imetoa pole kwa familia ya Zambi, jamaa na marafiki na kuwataka kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki cha msiba huo mzito.

    MSIMAMO WA LIGI KUU BARA

                                   P    W  D   L    GF       GA      GD     P
    Simba SC                3    3    -     -     7          1          6       9
    Azam FC                 3    2    1    -     3          1          2       7
    Coastal                    3    2    1    -     5          3          2       7
    JKT Oljoro               3    1    2    1    2          1          1       5
    Mtibwa Sugar          3    1    1    1    3          1          2       4
    Yanga SC               3    1    1    1    4          4          -        4
    Toto African            3    -     3    1    3          2          1       3
    Ruvu Shooting        3    1    -     2    4          5          -1     3
    African Lyon            3    1    -     2    2          5          -3     3
    JKT Ruvu                3    1    -     2    3          7          -4     3
    Prisons                   2    -     2    -     1          1          -        2
    Polisi Moro              3    -     2    1    -           1          -1     2
    Kagera Sugar         3    -     1    2    2          4          -2     1
    JKT Mgambo           3    -     -     3    1          3          -2     0
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM KURUDI KILELENI LIGI KUU LEO? Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top