• HABARI MPYA

    Monday, April 01, 2019

    BENZEMA AIFUNGIA BAO LA USHINDI REAL MADRID IKIILAZA 3-2 HUESCA

    Mshambuliaji Mfaransa, Karim Benzema akishangilia kishujaa baada ya kuifungia Real Madrid bao la ushindi dakika ya 89 ikiilaza Huesca 3-2 katika mchezo wa La Liga usiku wa jana Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid. Mabao mengine ya Real Madrid yamefungwa na Isco dakika ya 25 na Dani Ceballos dakika ya 62, wakati ya Huesca yalifungwa na Juan Hernandez dakika ya tatu na Etxeita dakika ya 74. Kwa ushindi huo, Real Madrid inafikisha pointi 57 baada ya kucheza mechi 29, ingawa inabaki nafasi ya tatu, sasa ikizidiwa pointi mbili na Atletico Madrid  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BENZEMA AIFUNGIA BAO LA USHINDI REAL MADRID IKIILAZA 3-2 HUESCA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top