• HABARI MPYA

    Wednesday, April 17, 2019

    AJAX YAITUPA NJE JUVENTUS LIGI YA MABINGWA

    Kinda mwenye kipaji wa Ajax, Matthijs de Ligt akishangilia baada ya kuifungia timu yake bao la ushindi dakika ya67 usiku wa jana Uwanja wa Allianz mjini Torino ikiwalaza 2-1 wenyeji, Juventus katika mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Ulaya. Cristiano Ronaldo alianza kuifungia Juventus dakika ya 28, kabla ya Donny van de Beek kusawazisha dakika ya 34 na kwa matokeo hayo, Ajax inakwenda Nusu Fainali kwa ushindi wa jumla wa 3-2 kufuatia sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza Amsterdam na itamenyana na mshindi wa jumla kati ya Tottenham na Manchester City 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AJAX YAITUPA NJE JUVENTUS LIGI YA MABINGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top