• HABARI MPYA

    Monday, April 15, 2019

    SOKA YA TANZANIA ILIVYOINUKA KWA KASI KIMATAIFA

    Na Hashim Mbaga, DAR ES SALAAM
    SOKA la Tanzania kwa muda huu imepanda sana kwa ujumla wake katika ramani ya soka barani Afrika.
    Timu zetu za Taifa na Club ya Simba Zimefanya Tuheshimike sana. Katika mambo yote lazima ukiona kitu kizuri ukitamani na ili uweze kukifanya lazima ujue takwimu za kufika pale zikoje.
    Kuna fact nyingi hebu tuangalie hizi kidogo zikoje:

    MASHINDANO YA CAF INTERCLUB
    Haya ni mashindano ambayo yanafanyika kila mwaka na mwaka huu Timu ya Simba imewakilisha nchi Vizuri mpaka hatua ya Quarter final CL na matunda yake yalikuwa haya
    - Wachezaji/Timu kupata EXPOSURE 
    - Timu kupata fedha za ziada Gate katika bajeti zao.
    - Tanzania kupata nafasi 4 za uwakilishi katika Caf interclub ya 2020/2021.

    TIMU 4 CAF INTERCLUB KWA TANZANIA
    Hii ndio mara ya kwanza Simba kutufanya Watanzania tuweze kupata uwakilishi wa Timu nne yaani 2 kwa Champions league na 2 kwa Confederation Cup katika mwaka wa kalenda ya CAF 2020/2021 inayoanza November 2020 katika historia yetu hili halitafutika.
    Hapa Simba imewafunulia Timu zingine za Tanzania kuweza kupata fursa ya Kimataifa.
    Katika kulienzi hili liendelee kwa muda inatakiwa kuanzia sasa msimu huu unaomalizika 2018/2019 mabingwa wa TPL na FA wapatikane Timu zilizo tayari kushindana sio kwenda kushiriki tu maana ili tuweze kupata nafasi zingine mfululizo wa kuingiza timu 4 kwa msimu 2021/2022 lazima timu hizi 2 za sasa Zinapokwenda kwenye Caf interclub 2019/2020 waingie Group Stage ili kupata Point zisizopingua 15 hadi 20 tukichanganya na points 14 tutakazobaki nazo baada ya kupungua kutoa 18 za msimu wa 2020/2021.
    Hivyo huu uwe mkakati wa Kitaifa ni lazima kuingia Group Stage hakuna dawa ingine zaidi ya hivyo zingine ni mbwembwe tu vinginevyo itakuwa tunarudi kuanza moja tena.
    Ndio maana sasa badala ya kutaniana au kukejeliana kwa matokeo ilitakiwa kupongezana na kukaa kwa pamoja kupata au kubadilishana mbinu kwa wote ili kufika target ya Kitaifa.

    MAFANIKIO KWA SIMBA
    Simba haijafika hapa ilipo kwa bahati mbaya iliweka mikakati na kuweka fedha. Ili kufika hatua hizi ni lazima uwe na mikakati kama ya Simba au zaidi na ili Simba iweze kuendelea hapa ilipofikia lazima itanue mikakati yake na bajeti ili kuendelea kuwa katika kiwango kizuri zaidi.

    Mfano hai:
    Bajeti ya Simba mwaka huu ilikuwa katika taswira hii

    MAPATO
    1. Sponsorship 1.7b
    2. Others Income 2b
    3. Soft loan 1.2b
    Total 4.9B

    MATUMIZI 
    1. Matumizi ya lazima 900k
    2. Salary & wages 2.7b
    3. Signing Fee & Bonus 1.2b
    4. Others exp 1.5b
    Total 6.3b

    Mpaka hapa kulikuwa na negative ya 1.4b katika ulinganifu wa bajeti.

    Bajeti iliyopo now baada ya kufikia mafanikio haya ipo/inakwenda katika taswira hii sasa

    MAPATO
    1. Sponsorship 1.7b
    2. Soft loan 1.2b
    3. Other Income 4.2b
    Total 7.1b
    Nb: Other Income zilizoongezekana ni kutoka International Match Gate Collection, Tv rights, Prizes.

    MATUMIZI 
    1. Matumizi ya lazima 1b
    2. Salary & wages 2.7b
    3. Sign fee & Bonus 1.8b
    4. Others exp 2b
    Total 7.5b
     NB hapa utaona kuna ongezeko katika Utawala, Bonus na Others.

    Ukiangalia Picha halisi hapo ya mfano wa bajeti ya mwanzo na ya pili utaona kabisa kuna vitu hivi
    1. Mapato yameongezeka
    2. Matumizi yameongezeka
    3. Negative imekuwa kubwa sana
    Haya ndio mafanikio ya Simba na ile Negative iliyopo pale inaweza kufidiwa kutoka katika mapato tarajiwa ya extra local Gate Collection, Simba Day, Uuzaji wa Jersey waziada hii itafanikiwa kama Simba watatwaa tena Ubingwa mwaka huu.

    MATARAJIO YA BAADAE
    Ili Timu zetu ziweze kufanikiwa kama  Simba nilazima tuwe na bajeti zinazoshabihiana na hizo hapo juu za Simba vinginevyo tutakuwa washiriki tu huo ndio ukweli.
    Na simba ili iendelee kuwa katika kiwango hiki na iweze kusonga mbele lazima bajeti yake ipande juu kuendana na uhalisia wavvitu unapotaka kuwa bingwa lazima ufanane na Mabingwa wenzako.

    Hapa Usajili, benchi la ufundi na miundombinu bila kusahau upande wa Utawala mabadiliko ni lazima kama kweli Simba inataka kufika hii nafasi iliyofika mwaka huu.

    TARGET TATAJIWA
    1. Kuchukua ubingwa TPL
    2. Kuingia group Stage 
    3. Kuwa na Mapato yasiyopungua 7.5b yaani ianzie pale ilipoishia kwenye matumizi ili Negative iwe kwenye Extra Income.
    4. Matumizi yake yanatakiwa kupanda ssanahasa kwenye Signing fee, Salary, bonus, others

    Mfano wa bajeti
    1. Matumizi ya lazima 1b
    2. Salary & wages 3.5b
    3. Sign fee & bonus 2.5b
    4. Others exp 2b
    Total 9b

    Hapa utakuwa unazungumzia Simba iliyokuwa tayari kwa semi final caf Interclub.
    Hapo unaona kabisa kuna negative ya 1.5b ili kuweza kukabiliana nayo hiyo nilazima kufanya vizuri ili uongeze Sporsorship, Prizes na Others Income kufidia mambo yote kadiri unavyokwenda juu na bajeti lazima ipande.

    WITO KWA WADAU WOTE
    Kwanza lazima tukubali mabadiliko katika mifumo yetu ya uuendeshajiwa timu na ligi li kuendana na wenzetu pili kutafuta vyanzo halisi vya mapato na mwisho nikuheshimu, kupongeza na kujifunza kutoka kwa alikutangulia ili kuweka chachu ya mafanikio miongoni mwetu sote kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla.
    Michezo inaleta amani furaha na upendo ndani ya jamii na mioyoni mwetu hivyo ina nafasi kubwa sana katika maisha yetu ya kila siku. VIVA TANZANIA, NI ZAMU YETU.
    (Mwandishi wa makala hii, Hashim Mbaga anapatikana kwa namba +255 764 100 001)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SOKA YA TANZANIA ILIVYOINUKA KWA KASI KIMATAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top