• HABARI MPYA

    Tuesday, April 16, 2019

    AUBAMEYANG AIREJESHA ARSENAL 'TOP FOUR' LIGI KUU ENGLAND

    Pierre-Emerick Aubameyang akishangilia baada ya kuifungia bao pekee Arsenal dakika ya 10 ikiwalaza wenyeji, Watford 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Vicarage Road huku akimaliza ukame wake wa mabao wa mechi saba. Watford ilimaliza pungufu baada ya Troy Deeney kutolewa kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwa kosa la kumpita Lucas Torreira dakika ya 11 tu na kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 66 sawa na Chelsea katika mchezo wa 33 na kurejea nafasi ya nne ikiizidi kwa pointi mbili Manchester United inayoshika nafasi ya sita 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AUBAMEYANG AIREJESHA ARSENAL 'TOP FOUR' LIGI KUU ENGLAND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top