Raheem Sterling akishangilia baada ya kuifungia Manchester City mabao mawili dakika za 15 na 63 katika ushindi wa 3-1 dhidi ya wenyeji, Crystal Palace leo kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Selhurst Park mjini London. Bao la tatu limefungwa na Gabriel Jesus dakika ya 90 wakati la Crystal Palace limefungwa na Luka Milivojevic dakika ya 81 na kwa ushindi huo Man City inafikisha pointi 83 baada ya kucheza mechi 33 na kurejea kileleni, ikiizidi pointi moja Liverpool ambayo muda inamenyana na Chelsea Uwanja wa Anfield katika mchezo wake wa 34 PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Park footballer kicks 22 GOALS in record 340 point Aussie Rules hammering -
and he was only filling in at forward to make up the numbers
-
An Adelaide Footy League club has put on a record flogging to kick off its
2024 season, with a midfielder turned forward blasting an incredible 22
goals in...
40 minutes ago
0 comments:
Post a Comment