• HABARI MPYA

    Friday, December 01, 2017

    MAKONDA, ABUBAKAR BAKHRESA WATEULIWA KAMATI ZA MAANDALIZI AFCON U17

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya Bakhresa Limited, Abubakar Bakhresa wameteuliwa kwenye Kamati za Maandalizi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 (AFCON U-17) mwaka 2019 nchini.
    Wakati Makonda, ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu, Abubakar Bakhresa ameteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kamati ya Usafiri na Malazi.
    Uteuzi huo umefanywa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), chini ya Rais wake, Wallace Karia na Makonda atasaidiwa na Makamu Mwenyekiti, Yusuph Singo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Michezo, Wajumbe Sunday Kayuni, Leslie Liunda, Nassoro Idrissa ‘Father’, Mohamed Kiganja ambaye ni Katibu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na Mhandisi Davis Shemangale.
    RC Paul Makonda ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu ya Maandalizi ya AFCON U17 mwaka 2019 nchini 

    Bakhresa atakuwa chini ya Mwenyekiti Mhandisi Ladislaus Matindi na Wajumbe Aziz Abood, Ahmed Mgoyi, Ahmed Shabiby, Dk. Maige Mwakasege Mwasimba na Shebe Machumani.
    TFF pia imeunda Kamati ya Masoko na Habari chini ya Mwenyekiti, Kelvin Twissa na Wajumbe Mwandishi wa Habari za Michezo na Katibu wa zamani wa TFF, Angetile Osiah, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Dk. Hassan Abbas, Dk. Omari Swaleh wa  Chuo Kikuu cha Mzumbe, Mkurugenzi wa AMG Group Iman Kajula na Mtendaji Mkuu wa Azam Media Limited, Tido Mhando.
    Kamati nyingine ni ya Fedha na Mipango itakayokuwa chini ya Mwenyekiti, Doto James na Wajumbe Mohamed Dewji, Dk. Seif Muba, Bernard Lubogo, Paul Bilabaye, Jacquelline Woiso na Cornel Barnabas.
    Kamati ya Uratibu Utalii itakuwa chini ya Mwenyekiti, Dk Khamis Kigwangala na Wajumbe , Allan Kijazi Devotha Mdachi ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Temeke, Hoyce Temu, Leah Kihumbi ambaye ni Mkurugenzi wa Sanaa na Makamu Rais wa zamani wa TFF, Athuman Nyamlani.
    Kamati ya Itifaki, Mwenyekiti ni Mndolwa Yusuph ambaye ni Kamishna Mkuu wa Uhamiaji na Wajumbe Filbert Bayi, Mkurugenzi Uwanja wa Ndege JNIA, Happiness Luangisa, Alex Makoye Nkenyenge na Alhaji Idd Mshangama.
    Kamati ya Tiba na Udhibiti wa Dawa za Kusisimua Misuli itakuwa chini ya Mwenyekiti, Profesa Lawrence Museru, Dk. Paul Marealle, Dk. Edmund Ndalama, Dk. Christina Luambano, Daktari Mkuu wa Hospitali ya Temeke na Hiiti Sillo.
    Kamati ya Sheria na Taratibu Mwenyekiti ni William Erio na Wajumbe Dk. Damas Ndumbaro, Edwin Kidifu, Ally Mayai na Khalid Abeid.
    Kamati ya Ulinzi na Usalama Mwenyekiti ni  IGP Simon Siro na Wajumbe Michael Wambura, CP. Andengenye wa Zimamoto, CP. Lazaro Mambosasa wa Polisi Kanda Maalum ya Dar-es-Salaam, Mkuu wa Askari wa Usalama Barabarani, TISS na Jonas Mahanga.
    Kamati ya Rasilimali Watu itakuwa chini ya Mwenyekiti Dk. Francis Michael, Allan Kijazi, Wane Mkisi, Juliana Yassoda na Gerald Mwanilwa.
    Kamati hizo ndogo zitakuwa chini ya Kamati Kuu inayoongozwa na Mwenyekiti Dk. Harrison Mwakyembe (MP); Makamu Mwenyekiti wa Leodegar Tenga na Mtendaji Mkuu wa Kamati hiyo ni Henry B. Tandau.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAKONDA, ABUBAKAR BAKHRESA WATEULIWA KAMATI ZA MAANDALIZI AFCON U17 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top