• HABARI MPYA

    Monday, December 25, 2017

    HUYU PIUS BUSWITA NI BONGE LA MCHEZAJI, YAANI ZAIDI YA FUNDI

    Kiungo wa Yanga, Pius Buswita akiivuta mpira ili kuinuka nao baada ya kuangushwa na mchezaji wa Reha FC, Abdul Hassan katika mchezo wa hatua ya 64 Bora michuano ya Azam Sports Federation Cup (ASFC)   
    Pius Buswita alianguka chini kabisa namna hii, lakini hakutaka kuupoteza mpira  
    Alifanikiwa kuinuka nao pamoja na kwamba Abdul Hassan aliendelea kuugombea
    Tazama namna miguu ya Pius Buswita inavyoshirikiana kwenye mpira, akimtoka kwa chenga tamu Abdul Hassan 
    Hapa Pius Buswita anapongeza baada ya kuifungia Yanga bao la kwanza dakika ya 82 kabla ya kumsetia Amissi Tambwe kufunga la pili dakika ya 84 katika ushindi wa 2-0 jana 
    Pius Buswita tena hapa dhidi ya Mohammed Abdallah wa Reha FC
    Pius Buswita akawekwa chini kwa rafu na Mohammed Abdallah na refa Heri Sasii anapuliza filimbi (kushoto)
    Pius Buswita anapiga mashuti huku anakimbia kwa kais na hatua kubwa. Yanga wamepata mchezaji mwingine mzuri wa safu ya kiungo baada ya kumpoteza Haruna Niyonzima aliyehamia kwa mahasimu, Simba SC msimu huu 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HUYU PIUS BUSWITA NI BONGE LA MCHEZAJI, YAANI ZAIDI YA FUNDI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top