• HABARI MPYA

    Thursday, October 12, 2017

    SHUGHULI PEVU MBAO FC NA MBEYA CITY MWANZA KESHO LIGI KUU

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea kesho Oktoba 13, 2017 kwa mchezo mmoja tu, wenyeji Mbao FC wakiikaribisha Mbeya City Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.
    Timu hizo ziko katika nafasi za katikati katika msimamo wa VPL, lakini ushindani unatarajiwa kuwa kwa timu za Simba SC, Mtibwa FC na Azam ambazo kila moja ina pointi 11 na ziko kileleni kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa tu.
    Ligi hiyo itaendelea Jumamosi, mabingwa watetezi, Yanga SC wakiwa wageni wa Kagera Sugar Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, Azam FC watakuwa wageni wa Mwadui FC kwenye Uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga na Ndanda watawakaribisha jirani zao, Maji Maji ya Songea Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara wakati Singida United itasafiri hadi Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi kucheza na wenyeji Ruvu Shooting ya Pwani.
    Majirani wengine, Njombe Mji na Lipuli ya Iringa watacheza kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe ilihali michezo mingine ya Ligi hiyo ikifanyika Jumapili Oktoba 15, ambako Simba itakuwa mwenyeji wa Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam wakati Tanzania Prisons itacheza na Stand United kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
    Ligi Daraja la Kwanza (FDL) nayo itaendelea ambako kesho kutakuwa na mchezo kati ya African Lyon na JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Timu hizo ni za Kundi A.
    Mechi nyingine kwenye kundi hilo itafanyika Jumamosi ambako Ashanti United itacheza na Mvuvumwa ya Kigoma kwenye Uwanja wa Uhuru ilihali Jumatatu Oktoba 16, Kiluvya itacheza na Friends Rangers kwenye Uwanja wa Uhuru huku Mgambo JKT ikishikamana na Mshikamano kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
    Kundi B kwa mujibu wa ratiba ni kwamba kesho Ijumaa JKT Mlale itacheza na Polisi Dar kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea huku michezo mingine katika kundi hilo ikicheza Jumapili kwa michezo mitatu.
    Siku hiyo Mbeya Kwanza itacheza na Mawenzi Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani, Coastal na Polisi Tanzania kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga huku Mufindi United itacheza na KMC Uwanja wa Samora mkoani Iringa.
    Kundi C litakuwa na mchezo mmoja siku ya Jumamosi  Oktoba 14, 2017 ambako Toto African itakipiga na Pamba kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na michezo mingine mitatu itafanyika siku ya Jumapili Oktoba 15, mwaka huu.
    Michezo ya Jumapili itakuwa ni kati ya Dodoma FC dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma; Rhino Rangers itacheza Biashara United wakati mchezo wa Alliance Schools na Transit Camp utachezwa kwenye Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.
    Ligi Daraja la Pili (SDL), Jumapili Oktoba 15, 2017 Kundi A kutakuwa mchezo kati ya Villa Squad na Abajalo FC Uwanja wa Kinesi, Dar es Salaam.
    Jumamosi kutakuwa na michezo miwili ya Kundi B ambako African Sports itacheza na Pepsi kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga huku Arusha FC itacheza na Kitayose kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.
    Jumapili Oktoba 15, 2017 katika kundi B hilo la B kutakuwa na mchezo mmoja kati ya Madini na Kilimanjaro Heroes kwenye Uwanja wa Nyerere mkoani Arusha.
    Kundi C kutakuwa na michezo yote mitatu ya raundi ya tatu ambako Ihefu itacheza na Green Warriors kwenye Uwanja wa Highland; Mkamba Rangers itacheza na The Mighty Elephant kwenye Uwanja wa Mkamba huko Morogoro ilihali Boma FC dhidi ya Burkinafaso zitacheza Uwanja wa Mwakangale, Mbeya.
    Kundi D pia kutakuwa na mechi zote tatu Oktoba 14, 2017 ambako Nyanza itacheza na Mashujaa kwenye Uwanja wa Nyerere; Area ‘C’ United itacheza na Milambo Uwanja wa Jamhuri Dodoma wakati JKT Msange itacheza na Bulyanhulu kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SHUGHULI PEVU MBAO FC NA MBEYA CITY MWANZA KESHO LIGI KUU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top