• HABARI MPYA

    Sunday, August 12, 2018

    RONALDO AFUNGUA AKAUNTI YA MABAO JUVENTUS IKIUA 5-0

    Mshambuliaji Cristiano Ronaldo akiifungia timu yake mpya, Juventus bao la kwanza leo dakika ya nane katika mchezo wa kirafiki dhidi ya timu yao ya vijana chini ya umri wa miaka 19 kabla ya kusababisha bao la kujifunga kwa wadogo zao hao katika ushindi wa 5-0. Mabao mengine yalifungwa na Paulo Dybala mawili na Claudio Marchisio. Mreno huyo mwenye umri wa miaka 33 alikuwa anaichezea kwa mara ya kwanza timu hiyo iliyomnunua kutoka Real Madrid kwa dau la Pauni Milioni 100 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO AFUNGUA AKAUNTI YA MABAO JUVENTUS IKIUA 5-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top