• HABARI MPYA

    Thursday, October 29, 2015

    MAN CITY NA LIVERPOOL ZAMSOGELEA ‘MWALI’ WA CAPITAL ONE ENGLAND, ARSENAL NJE

    MATOKEO NA RATIBA KOMBE LA LIGI ENGLAND:
    Oktoba 28, 2015  
    Manchester United (1) 0 - 0 (3) Middlesbrough
    Manchester City 5 - 1 Crystal Palace
    Liverpool 1 - 0 Bournemouth
    Southampton 2 - 1 Aston Villa
    Oktoba 27, 2015  
    Sheffield Wednesday 3 - 0 Arsenal
    Stoke City (5) 1 - 1 (4) Chelsea
    Everton (4) 1 - 1 (3) Norwich City
    Hull City (5) 1 - 1 (4) Leicester City
    Desemba 1, 2015
    Middlesbrough v Everton Riverside 
    Southampton v Liverpool
    Manchester City v Hull City
    Stoke City v Sheffield Wednesday 
    Nahodha wa Manchester City, Yaya Toure akifunga bao la nne jana dhidi ya Crystal Palace PICHA ZAIDI GONGA HAPA

    MANCHESTER City na Liverpool zimekwenda Robo Fainali ya Kombe la Ligi England, maarufu kama Capital One Cup kufuatia ushindi kwenye mechi zao za jana usiku, huku Manchester United ikiungana na Arsenal kuaga michuano hiyo.
    Manchester United imetolewa kwa penalti 3-1 na Middlesbrough baada ya sare ya 0-0 Uwanja wa Old Trafford, wakati Manchester City imeshinda 5-1 dhidi ya Crystal Palace Uwanja wa Etihad.
    Mabao ya City yamefungwa na Wilfried Bony dakika ya 22, Kevin De Bruyne dakika ya 44, Kelechi Iheanacho dakika ya 59, Yaya Toure kwa penalti dakika ya 76 na Manuel Garcia Alonso dakika ya 90 na ushei, wakati bao la kufutia machozi la Palace limefungwa na Damien Delaney dakika ya 89.
    Bao pekee la Nathaniel Clyne dakika ya 17 limeipa 
    Liverpool ushindi wa 1-0 dhidi ya Bournemouth Uwanja wa Anfield, wakati Southampton imeichapa 2-1 Aston Villa mabao ya Maya Yoshida dakika ya 51 na Graziano Pelle dakika ya 77, bao la wageni likifungwa na Scott Sinclair kwa penalti dakika ya 90 na ushei Uwanja wa St. Mary's.
    Mapema juzi, Sheffield Wednesday iliikung’uta 3-0 Arsenal, mabao ya Ross Wallace dakika ya 27, Lucas Eduardo Santos Joao dakika ya 40 na Sam Hutchinson dakika ya 51 Uwanja wa Hillsborough.
    Chelsea nayo ilitolewa kwa penalti 5-4 baada ya sare ya 1-1 na Stoke City Uwanja wa Britannia. Stoke walitangulia kwa bao la Jonathan Walters dakika ya 52, kabla ya Loic Remy kusawazisha dakika ya mwisho.
    Everton iliitoa Norwich City kwa penalti 4-3 baada ya sare ya 1-1 Uwanja wa Goodison Park na Hull City iliitoa Leicester City kwa penalty 5-4 baada ya sare ya 1-1 Uwanja wa The KC.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN CITY NA LIVERPOOL ZAMSOGELEA ‘MWALI’ WA CAPITAL ONE ENGLAND, ARSENAL NJE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top