• HABARI MPYA

    Monday, October 19, 2015

    AZAM FC WAIFUATA NDANDA MTWARA, YANGA WATAKUWA NA ‘TOTO LAO’ TAIFA JUMATANO, SIMBA WANABAKI MBEYA NA MAAFANDE

    MATOKEO NA RATIBA LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA
    Okotba 17, 2015
    Yanga SC 1-1 Azam FC
    Majimaji FC 1-0 African Sports
    Mbeya City 0-1 Simba SC
    Ndanda FC 0-0 Toto Africans
    Stand United 3-0 Prisons
    Coastal Union 0-1 Mtibwa Sugar
    Oktoba 18, 2015
    Mgambo Shooting 2-0 Kagera Sugar
    Mwadui FC 2-1 JKT Ruvu
    MECHI ZIJAZO..
    Oktoba 21, 2015
    Yanga SC Vs Toto Africans
    Stand United Vs Majimaji FC
    JKT Ruvu Vs Mtibwa Sugar
    Prisons Vs Simba SC
    Coastal Union Vs Kagera Sugar
    Oktoba 22, 2015
    Ndanda FC Vs Azam FC
    Mwadui FC Vs Mgambo Shooting
    Mbeya City Vs African Sports
    Mziki wa Azam FC unahamia Nangwanda Sijaona Alhamisi dhidi ya Ndanda FC

    Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
    KIKOSI cha Azam FC kinatarajiwa kuondoka kesho Dar es Salaam kwenda Mtwara kwa ajili ya mchezo wao ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Alhamisi dhidi ya wenyeji, Ndanda FC.
    Baada ya sare ya 1-1 na mabingwa watetezi, Yanga SC, Azam FC wamepania kufufua wimbi lao la ushindi keshokutwa mjini Mtwara.
    Azam FC ambao walilalamikia uchezeshaji mbovu wa refa Abadallah Kambuzi wa Shinyanga Jumamosi dhidi ya Yanga SC, wataendelea kumkosa kocha wao, Muingereza Stewart John Hall siku hiyo uwanjani kwa sababu bado anatumikia adhabu yake ya kadi nyekundu aliyoonyeshwa katka mchezo dhdi ya Coastal Union.
    Stewart atasafiri na timu na kuiandaa kama kawaida mazoezini, lakini siku ya mechi atakuwa jukwaani na mashabiki wengine kuangalia mchezo.
    Azam FC inafukuzana na Yanga SC kileleni mwa Ligi Kuu, kila timu ikiwa na pointi 16 baada ya kucheza mechi sita, wakifuatiwa na Simba SC wenye pointi 15.
    Kwa ujumla, Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea katikati ya wiki, Yanga SC wakiwakaribisha wanawe Toto Africans Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Stand United na Majimaji FC Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, JKT Ruvu na Mtibwa Sugar Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, Prisons na Simba SC Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya na Coastal Union na Kagera Sugar Uwanja wa Mkwakwani, Tanga Jumatano.
    Ligi Kuu itaendelea tena Alhamisi, Ndanda FC wakiwa wenyeji wa Azam FC Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara, Mwadui FC ikimenyana na Mgambo Shooting Uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga wakati Mbeya City watakuwa wenyeji wa African Sports ya Tanga.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC WAIFUATA NDANDA MTWARA, YANGA WATAKUWA NA ‘TOTO LAO’ TAIFA JUMATANO, SIMBA WANABAKI MBEYA NA MAAFANDE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top