• HABARI MPYA

    Thursday, October 29, 2015

    TAIFA STARS KUIFUATA ALGERIA KWA 'DEGE' LA KUKODI

    TIMU ya soka ya taifa Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, inatarajiwa kusafiri na ndege ya binafsi ya kukodi ya shirika la Fastjet kuelekea nchini Algeria kwa ajili ya mchezo wa marudiano utakaochezwa Novemba 17 mjini Algiers.
    Meneja Mkuu wa Shirika la Ndege la Fasjet kwa ukanda wa Afrika Mashariki, Jimmy Kibati amesema kampuni yao imefikia makubaliano na TFF ya kuwa msafirishaji rasmi wa timu ya Taifa kwa ajili ya mchezo huo wa kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia nchini Urusi 2018 dhidi ya Algeria.

    Jimmy amesema katika safari hiyo, Fastjet itatoa ndege yenye uwezo wa kubeba abiria 156 walioketi, sambamba na wafanyakazi wa ndenge, ambapo wao wametoa punguzo la asilimia 35 katika gharama nzima ya safari ya kuelekea Algeria.
    Aidha Jimmy ameongeza kuwa safari hiyo itakua ni ya masaa 7 ambapo ndege ikitoka Dar es salaam itatua Djamena – Chad kuongeza mafuta kabla ya kuendelea tena na safari mpaka nchini Algeria.
    Naye katibu wa kamati ya Taifa Stars, Teddy Mapunda aliwashukuru Fastjet kwa kukubali kuwa wasafirishaji rasmi wa TaifA Stars kwa mechi dhidi ya Algeria, huku akisema gharama za safari za mtu mmoja kusafiri ni dolla 800 kwenda na kurudi.
    Teddy amewaomba watanzania, wapenzi, washabiki wa mpira wa miguu wanaotaka kusafiri kufika ofisi za TFF zilizopo Karume kwa ajili ya kujiandiksha na kuelekea taratibu nzima za safari.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA STARS KUIFUATA ALGERIA KWA 'DEGE' LA KUKODI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top