• HABARI MPYA

    Friday, February 24, 2012

    TFF YAWAPA 'ILIMU' MADOKTA WA MICHEZO

    Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeandaa kozi ya awali ya madaktari au wataalamu wa viungo (physiotherapist) kwa klabu za Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza itakayofanyika jijini Dar es Salaam.
    Kozi hiyo ya siku tano itakayoanza Machi 5-9 mwaka huu itakuwa na washiriki 32 tu. Kila klabu inatakiwa kutuma mshiriki mmoja ambapo anatakiwa kuwa daktari wa timu au physiotherapist.
    Katika sifa za kitabibu, washiriki wanatakiwa wawe Clinical Officer (Medical Assistant), Assistant Medical Officer na Medical Officer au Physiotherapist. Ada ya kushiriki ni sh. 60,000.
    Washiriki wanatakiwa kutuma TFF wasifu wao (CV) na nakala za vyeti vyao vya kitaaluma na mwisho wa kuthibitisha kushiriki kozi hiyo ni Machi Mosi mwaka huu. Kwa madaktari wanatakiwa wawe ambao kwa sasa wanazitumia klabu husika (active).
    Kila klabu itamgharamia mshiriki wake kwa malazi, nauli ya kuja na kurudi pamoja na posho wakati TFF itatoa vifaa vya kozi (stationeries), chai na chakula cha mchana.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TFF YAWAPA 'ILIMU' MADOKTA WA MICHEZO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top