• HABARI MPYA

    Tuesday, February 28, 2012

    AVB TUMBO JOTO CHELSEA



    ANDREVILLAS-BOAS amekiri kuwa huenda akatupiwa virago vyake na mmliki wa klabu yaChelsea, Roman Abramovich. Kocha huyo amekuwa kwenye hofu kubwa kama bilioneahuyo atamuunga mkono na anahisi kuwa zamu yake ya kutumuliwa ‘kimbwa koko’ inakaribia,kama alivyofanyiwa aliyemrithi mikoba Carlo Ancelotti.


    Kocha huyowa Ureno, ambaye alikuwa akitangza kuungwa mkono na Abramovich amesema: “Kwasasa tuko katika kipindi kama kile cha mwaka jana. Ni nakala ya mwaka jana.”

    “Nafikirikwamba sasa tunaujasiri kwa Abramovich. Lakini tabia yake ya kuwashughulikia makochakatika hali tuliyonayo au hata nzuri. Ni nini kitafuata? Itakuwa ni kati ya lakwanza au la pili — kuendelea na kazi na kuungwa mkono au tabia yake ya kilawakati. Hatujui.”

    AVB, mwenyeumri wa miaka 34, amekuwa katika hofu kubwa kutokana na matokeo mabaya nakugombana na wachezaji wa zamani kama Frank Lampard na Ashley Cole.

    Wachezajiwote wawili wa England walianzia benchi katika mechi ya Ligi ya Mabingwa dhidiya Napoli na Lampard kusema kuwa uhusiano wake na AVB ni wa kivile.

    AVB anaasilimia 17 ya ushindi kwenye mechi zake sita, wakati Ancelotti alikuwa na 50 akishikanafasi ya pili Mei mwaka jana.

    Lakini kamaatabahatika kubaki Stamford Bridge, Villas-Boas amepanga kukijenga kikosi chakekwa jinsi atakavyoweza yeye na si kama alivyofanya kocha Roberto Mancini kwatimu yake ya Manchester City.

    Alisema:“Nakataa kujenge timu kama Manchester City. Sivutiwa na kiwango chao cha soka.City ni timu ya Taifa ya Italia na iko kwenye kiwango hicho.”

    “Kamaunavyomuona Frank Lampard, hayuko kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo kwasababu za sera zake za timu. Lakini ni mmoja wa wachezaji bora.”

    AVB anawatazamawachezaji wake wa baadaye kama Hulk kutoka kwenye klabu yake ya zamani Porto.

    Alisema:“Naona nafasi kwa wachezaji wenye nguvu hasa kwa upande wa winga, ambaowatakuwa na nguvu ya kuvaana mtu mmoja kwa mmoja na Hulk anastahili kwenyenafasi hiyo.”Pia anamtakakiungo wa Porto Joao Moutinho na winga na beki Alvaro Pereira.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AVB TUMBO JOTO CHELSEA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top