• HABARI MPYA

    Tuesday, February 21, 2012

    KAMATI YA SHERIA NA MAADILI YA TFF...


    Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ilikutana Februari 15 mwaka huu jijini Dar es Salaam na kufanya uamuzi kwa ajenda mbalimbali ikiwemo Marekebisho ya Katiba za Wanachama wa TFF, na pia ushauri wa kisheria ulioombwa kwake na Kamati ya Uchaguzi ya TFF.
    Uamuzi uliofanywa kwa wanachama wote 40 wa TFF ni ufuatao; wanachama wote wanatakiwa kufanya marekebisho kwenye katiba zao katika maeneo matatu kwa mujibu wa maelekezo ambayo TFF ilitoa mwaka jana.
    Maeneo hayo ni sifa za wagombea uongozi ambapo kwenye kipengele cha elimu ni lazima iwe kuanzia kidato cha nne, kutopeleka masuala ya mpira wa miguu katika mahakama za kawaida na kamati zao za uchaguzi kufanya kazi chini ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF.
    Hivyo hakuna mwanachama yeyote wa TFF anayeruhusiwa kufanya uchaguzi kwa sasa kama katiba yake ina upungufu au inakwenda kinyume na maelekezo kuhusu maeneo hayo matatu.
    Kamati imetoa hadi Juni Mosi mwaka huu kwa wanachama ambao katiba zao zina upungufu katika maeneo hayo wawe wamefanya marekebisho ndiyo waendelee na uchaguzi kwa wale ambao muda wa uchaguzi umefika.
    Ushauri wa Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji kwa Kamati ya Uchaguzi ya TFF ni kuwa katiba zote za wanachama ziwe na vitu hivyo vitatu.

    Alex Mgongolwa
    Mwenyekiti
    Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KAMATI YA SHERIA NA MAADILI YA TFF... Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top