WAKATI tamasha maalum kwa vyombo vya habari ‘Media Day’ kwa mwaka 2012 likipangwa kufanyika Machi 24
kwenye ufukwe wa Msasani, Kampuni ya bia
Tanzania (TBL) imetoa shilingi mil.62.5 kwa ajiliya kudhamini tamasha hilo.
Mkurugenzi wa
Uhusiano wa Jamii na Sheria wa TBL Steven Kilindo alisema kuwa wameamua
kudhamini tamasha hilo kutokana na kuthamini mchango wa waandishi wa habari
katika biashara za kampuni yao.
“TBL itahakikisha bonanza la mwaka huu linafana na litakuwa
la aina yake kuanzia katika michezo, burudani, vinywaji na vyakula, hivyo
tunawaomba waandishi wajitokeze kwa wingi ili kuweza kubiridika pamoja na kubadilishana
mawazi,”Alisema Kilindo.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo
(TASWA) ambayo ndiyo waandaaji wa bonanza hilo
Juma Pinto, pamoja na kuishukuru TBL kwa udhamini huo aliiomba kutoishia
kudhamini kwenye mabonanza tu bali wafanye hivyo hata katika mafunzo mbalimbali
yanayoaandaliwa na chama hicho.
0 comments:
Post a Comment