• HABARI MPYA

    Friday, February 24, 2012

    BEKI LA YANGA LAPEWA UNAHODHA THE CRANES

    BEKI aliyewahi kufanya mazungumzo na Yanga, lakini wakashindana mwaka 2005, Andrew Mwesigwa ameteuliwa kuwa Nahodha mpya wa timu ya taifa ya Uganda, The Cranes akichukua nafasi ya Ibrahim Sekagya aliyetangaza kustaafu mapema wiki hii. Uteuzi huo umefanyika baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Uganda (FUFA), kilichofanyika leo asubuhi kwenye Uwanja wa Namboole.
    Simon Masaba wa URA ameteuliwa kuwa Nahiodha Msaidizi wa Mwesigwa, ambaye Nahodha Msaidizi kwa muda mrefu.
    Awali alichezea SC Villa ya Uganda kati ya mwaka 2002 na 2005 kabla ya kujiunga na  IBV ya Iceland ambako alicheza misimu mitatu 2006-2009 alipotimkia Chongqing ya China mwaka 2010 kisha kutua FC Odarbasy ya Kazakhtan mwaka jana.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BEKI LA YANGA LAPEWA UNAHODHA THE CRANES Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top