KLABU ya soka ya Simba inatarajiwa kufanya hafla ya uzinduzi
wa Simba Tv ambao unatarajiwa kufanyika Ijumaa katika hoteli ya JB Belmont
iliyopo katika jengo la Benjamin Mkapa katikati ya jiji la Dar es Salaam.
Ofisa habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga amesema kwamba Simba
Tv itakuwa ikirushwa katika kituo cha Clouds Tv.
Alisema
kupitia uzinduzi huo kutakuwa na burudani mbalimbali sambamba na kuonyeshwa kwa
documentary maalum inayohusu klabu hiyo.
"Hafla
hii itakuwa ni kwa waalikwa huku wengine watakaopenda kuhudhuria watapaswa
kulipa shilingi 70,000.
0 comments:
Post a Comment