• HABARI MPYA

    Tuesday, February 21, 2012

    BRAZAMENI HAYE ATIMKIA MAREKANI BAADA YA KUIBUA TIFU NA CHISORA MUNICH

    Bondia Muingereza David Haye, katikati, akiwa na rafiki zake wakipita katika Uwanjua wa Ndege wa Heathrow, London kuelekea Marekani jana. Haye aligombana na bondia mwenzake wa Uingereza, Dereck Chisora aliyetoka kuzipiga na Vitali Klitschko, mjini Munich, Ujerumani Jumamosi. Bodi ya Ngumi Uingereza inafanya uchunguzi juu ya tukio hilo juu ya Chisora na ikibainika atachukuliwa hatua.  Haye hawezi kuchukuliwa hatua, kwa sababu bondia huyo wa London amestaafu ndondi mwaka jana baada ya kupiwa na mdogo wake Klitschko, Wladimir, lakini inaaminika Haye anatafutwa na Polisi wa Ujerumani kwa mahojiano juu ya tukio hilo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BRAZAMENI HAYE ATIMKIA MAREKANI BAADA YA KUIBUA TIFU NA CHISORA MUNICH Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top