• HABARI MPYA

    Saturday, February 25, 2012

    BALOTELLI ATUPIA, WBA YAIPIGA 4-0 SUNDERLAND

    KLABU ya Wigan walilazimishwa sare ya bila kufungana na Aston Villa kwenye Uwanja wa DW Stadium.
    Aidha, bao pekee la Pavel Pogrebnyak lilitosha kuipa Fulham iliyocheza pungufu ya mchezaji mmoja ushindi wa 1-0 dhidi ya Queens Park Rangers kwenye Uwanja wa Loftus Road.
    Katika mchezo mwingine, West Bromwich Albion iliibuka na ushindi wa kwanza ndani ya miezi mitatu ilipoitandika mabao 4-0 nyumbani Sunderland 4-0.
    Wiki mbili tangu ipate ushindi mkubwa zaidi ugenini msimu huu wa mabao 5-1 dhidi ya Wolverhampton, West Brom ilipata mabao mawili kila kipindi dhidi ya Sunderland.
    Peter Odemwingie, aliyepiga mabao matatu peke yake dhidi ya Wolves, jana alifunga bao la mapema kabla ya James Morrison kufunga linguine kabla ya mapumziko na Keith Andrews, ambaye alicheza mechi ya kwanza dhidi ya timu yake ya zamani, Wolves alifunga dakika za lala salama.
    West Brom haikuruhusu nyavu zake kuguswa kwa mara ya kwanza ndani ya miezi miwili. Mechi kati yua Man City na Blackburn Rovers inaendelea Etihad Stadium na tayari Balotelli amekwishatupia. Manchester
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BALOTELLI ATUPIA, WBA YAIPIGA 4-0 SUNDERLAND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top