• HABARI MPYA

    Friday, February 24, 2012

    JOHN BOCCO NA HUSSEIN JAVU NDIO MA STRIKER WA KUTAYARISHWA KUIBEBA STARS

    John Bocco wa Azam na Hussein Javu wa Mtibwa Sugar, nchi inahitaji kuwekeza kwa wachezaji hawa ili wawe washambuliaji tegemeo wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars. Hawa watu wanahitaji kulishwa vitu vya zaida ambavyo wanakosa sambamba na elimu ya  kujitambua, waache ulimbukeni wa kulewa sifa, wawe na malengo ya kufika mbali, ili wajibidiishe zaidi. Ni watu ambao wanaweza kazi na kama taifa litaamua kuwekeza kweli kwa watu hawa, tutakuwa na miaka mitatu ya kushangilia mabao yao. Watu wanaweza kuufanya mpira ukae kwenye eneo la wapinzani. Wana uwezo. Tuwape nafasi na tuwape muda kabla ya kuanza kula matunda yao.     
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JOHN BOCCO NA HUSSEIN JAVU NDIO MA STRIKER WA KUTAYARISHWA KUIBEBA STARS Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top