• HABARI MPYA

    Monday, February 20, 2012

    HUNTELAAR AING'ARISHA SCHALKE BUNDESLIGA

    MSHAMBULIAJI Klaas-Jan Huntelaar alifunga mabao mawili na kuisaidia Schalke kuilaza Wolfsburg mabao 4-0 katika Bundesliga jana. Huntelaar pia alipiga penalti iliyookolewa na kipa wa Wolfsburg, Diego Benaglio. Huntelaar sasa analingana na Mario Gomez wa Bayern Munich kwa mabao, kila mmoja 18 na Schalke inaongoza Bundesliga kwa jumla ya mabao 50.
    Hannover iliifunga Stuttgart 4-2, Christian Pander akifunga moja na kupika mawili.
    Borussia Dortmund inaongoza ligi hiyo ikiizidi pointi tatu Borussia Moenchengladbach.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HUNTELAAR AING'ARISHA SCHALKE BUNDESLIGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top