• HABARI MPYA

    Saturday, February 24, 2018

    SALAH AFIKIA REKODI YA MABAO YA SUAREZ LIVERPOOL MAPEMAA

    MSHAMBULIAji wa kimataifa wa Misri, Mohamed Salah ameendeleza mwanzo wake mzuri Liverpool baada ya leo kufikia rekodi ya mabao ya mchezaji wa zamani wa klabu hiyo, Luis Suarez ya kufunga mabao 31 kwa msimu.
    Kwa kufunga leo kwenye ushindi wa 4-1 dhidi ya West Ham United Uwanja wa Anfield, sasa amefikia idadi ya mabao ambayo nyota wa Uruguay, Suarez alifunga katika msimu wake wa mwisho Liverpool, 2013-14.
    Suarez ambaye baada ya hapo alihamia Barcelona, alifunga mabao hayo 31 katika mechi 37, kama Salah msimu huu.
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 amefikisha rekodi hiyo mapema zaidi ya Suarez kwa sababu Liverpool ya Salah inacheza mashindano zaidi, ikiwemo Ligi ya Mabingwa.

    Mohamed Salah leo amefikia rekodi ya mabao ya Luis Suarez Liverpool
     PICHA ZAIDI GONGA HAPA 

    LUIS SUAREZ'S RECORD IN 2013-14 

    Mechi alizocheza: 37
    Mabao aliyofunga: 31 
    Pasi za mabao: 14
    Nafasi alizotengeneza: 101 

    REKODI YA MOHAMED SALAH MSIMU HUU 

    Mechi alizocheza: 37
    Mabao aliyofunga: 31 
    Pasi za mabao: 9
    Nafasi alizotengeneza: 62 


    Luis Suarez anayechezea Barcelona kwa sasa, msimu wa 2013-2014 alifunga mabao 31 katika mechi 37 Liverpool
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SALAH AFIKIA REKODI YA MABAO YA SUAREZ LIVERPOOL MAPEMAA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top